Thursday, September 27, 2012

Mji wa Mafia (Kilindoni) na viunga vyake.

Nauliza hivi! Mafia si mji wa utalii!!? Inakuwaje mwaliacha soko la mji huu kuwa chafu kiasi hiki? Haya siyo maji yaliyotuama kwa sababu ya mvua maana msimu wa mvua kisiwani hapa bado, lakini ni maji kutoka kwenye vibanda vya 'Mama Lishe' walioko ndani ya soko kuu la Mafia. Simo humu naapa.

Tungali bado kwenye viunga vya mji wa Mafia na hapa ni sokoni. Ha ha ha ha ha ha!!! Nicheke ninenepe Chokoraa wa watu.
Huku ni mwendo wa "ushungi" aisee, Usije na vimini na vipedo vyenu mnavyovalishana mkituonyesha siri zenu enyi wana na humu mi simo.

Chokoraa nilipata pia nafasi ya kutembelea ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Mafia na hili ndilo jengo la "Muishiwa" huyu. Ha ha ha ha ha! Ati hapo inapopepea bendera ya kaya yetu hii, miaka kadhaa kabla ya 1961 ilipepea bendera ya "mkoloni". Simo humu miye.

Usiache kunitumia barua na hata kifurushi kutokea huko kwenu ughaibuni kwa anuani ifuatayo: Mheshimiwa Chokoraa wa Muhangaikaji wa Mlalahoi wa Pangupakavu wa Kabwela wa Mdanganyika, S.L.P .....Mafia, Pwani ya Wadanganyika. Pia biashara ya kuuza vocha inaendelea hapa na mimi nauliza haya makampuni ya simu yanalipia ushuru!!!!? Simo.
'Prezidenti' wa Wilaya, D.C ama ukipenda Mkulu wa Kaya wa Mafia ana ofisi zake hapa na hili lote ni jengo la ofisi za "muishiwa" huyu. Ati! Mtu mmoja jengo lote hili na mwalimu aliwahi kuuliza "...kwani mi tembo?". Na hii je!!!!!? Sihusiki naapa, simo.
Usitie shaka kuja na Njuluku, Pesa, Sinyingi, Hela, Chokoraa naita "Shekeli" zako huku kwetu maana hata sisi tunayo "Nyumba ya hela" na inayo "Ei tii Emu" inayofanya kazi saa 24 mfululizo. Sihusiki bado.
Uwanja wa ndege wa Mafia. Jengo hili halitumiki kwa sasa kwa sababu uwanja uko kwenye matengenezo makubwa ukitarajiwa kuwa na jengo la kisasa kabisa lakini hii ndiyo hali halisi miaka 50 baada ya uhuru. Sihusiki mimi humu..
'Muishiwa' Batuli, Diwani wa Kata ya Kirongwe, Kata ya Kaskazini Mafia akielezea jambo tulipokutana naye kwenye kijiji cha Jimbo huko Mafia. Wa kwanza kulia ni Dk. Kiwia, mtaalamu wa Uvuvi wenyewe twaita Fisheries. Nahusika kwani miye humu!!!? Simo.
 Dk. Kiwia kutoka Fisheries, Ndg Makongoro mtaalamu wa mazingira, Chokoraa wa Muhangikaji wa Mlalahoi wa Pangupakavu wa Kabwela wa Mdanganyika, 'Muishiwa Diwani wa Kirongwe, Muishiwa Mwenyekigoda wa Kijiji cha Banja wakimsikiliza mwananchi akidadavua mada kwenye mkutano. Ha ha ha ha ha!!! Nijitoe na humu?. Simo.

FOTOA FOTO YA CHOKORAA KISIWANI MAFIA.

Nasema humu Chokoraa sihusiki na simo tena simo kabisaaaaa!!! Ala! Nani kakwambia Chokoraa nakaa jalala moja!? Nilikwenda kisiwa cha Mafia juma lililopita na katika pita pita yangu kwenye majalala yangu nikakutana na hali hii, nikaamua kufanya katabia kangu kaleeee ka zamani nilikokatazwa nisisikie yaanI "FOTOA FOTO". We kuwamo humu japo mi simo tena simo kabisaaaaaaa.
Kwanza ni "Usafiri" wetu. Hapa kwetu Mafia hatuna "Teksi" na wala huo upuuzi wenu wa kutumia magari hata kwa safari fupi kisa mwaonyesha ufahari wa kuwa na mafedha kedekede sisi hatumo na humu Chokoraa nilikataa kuhusika. Kuna njia mbili tu za kuingia kisiwa hiki chenye utajiri wa mali na utu na mara unapofika ama kwenye bandari yetu kongwe isiyoendelezwa bado ukitumia usaifiri wa "boti" kutokea Nyamisati au wale "waishiwa" msiochoka kuishiwa mkijifanya kutumia "ulozi wa ndhungu" kwa kupanda 'ungo' mchana kweupeeeee! Na humo simo, hata hivyo usaifiri wako wa kuzunguka mjini humu ni pikipiki iwe ya matairi mawili almaarufu "Bodaboda" ama matairi matatu almaarufu "Bajaji". Teksi zenu tupa kule!!! Simo nasema.
Halafu! Huku kwetu ule uchafu wenu muutiao barabarani mkiifanya nyeusi tiii kama mkaa ati wenyewe mwaita lami huku sisi upuuzi huo hatuna hata mmoja. Huu mji wa kitalii bwana lazima uwe "nechuro". Ha ha ha ha ha ha!!! Sihusiki miye humu naapa.
Halafu nani kasema ati wanawake wa Pwani hawajui kutafuta pesa ila akina "Manka" peke yao!!!? Nyooo!! Simo. Hapa kwetu sokoni kwa lugha ya 'Ami' yangu wa kule Mchambawima paitwa "Malikiti" akina mama wanauza kitoweo. Yaani akina baba wavua, na akina mama wauza na wote watia kipato ndani ya nyumba sasa hilo la haki sawa mwalikataa kwanini!!!? Simo humu miye.


"Si hasa" za Kaya yetu nazo zatuhusu na sisi twahusika. Hapa ni kikao cha kamati za vijiji vya Banja na Jojo kilichofanyika shule ya msingi Banja ambapo wanavijiji hawa walikutana na wataalamu wa mazingira na hapa mmoja wa wanakamati akihoji swali na kutoa maoni yake. Ha ha ha ha ha!! Nisifurahi kwanini Chokoraa miye.


Kwenye kikao hiki, ndugu yenu Chokoraa wa Muhangaikaji wa Mlalahoi wa Pangupakavu wa Kabwela wa Mdanganyika nilikaribishwa niketi na mimi pamoja na wakuu na sikufungua kinywa kunena bali kusikiza yale yaliyosemwa na wana kaya maana simo.

 Huyu si mgonjwa jamani kwamba anakandwa mkono umevunjika ama kakutwa na madhila. La hasha! Anapambwa mtoto wa kike kabla ya harusi na kama huyajui haya basi hujafika Pwani weye na mi humo simo, tena simo kabisaaaaaaaa.

 Haya tena, kishapendeza mtoto wa kike asubiriwa somo hapa mambo yaanze. Ha ha ha ha ha ha! Tembea ulishe macho yako wewe! Kila siku kumshangaa Chokoraa, ohoo! mara Chokoraa ana maneno mengi! Si nimeona mengi!!!? Simo humu miye.

Somooooooooo!!!! Yuko wapi somoye harusi jamani aje hapa tuhangaike naye, nasema aje hapaa, nasema aje hapaa, nasema aje hapaaa!!!!!!!! Nahusika humu kwani miye!? Simo.



Haya, kwa leo nakomea hapa. Ni mimi ndugu yenu Chokoraa wa Muhangaikaji wa Mlalahoi wa Pangupakavu wa Kabwela wa Mdanganyika, nawasiliamia.