Nauliza hivi! Mafia si mji wa utalii!!? Inakuwaje mwaliacha soko la mji huu kuwa chafu kiasi hiki? Haya siyo maji yaliyotuama kwa sababu ya mvua maana msimu wa mvua kisiwani hapa bado, lakini ni maji kutoka kwenye vibanda vya 'Mama Lishe' walioko ndani ya soko kuu la Mafia. Simo humu naapa.
Tungali bado kwenye viunga vya mji wa Mafia na hapa ni sokoni. Ha ha ha ha ha ha!!! Nicheke ninenepe Chokoraa wa watu.
Huku ni mwendo wa "ushungi" aisee, Usije na vimini na vipedo vyenu mnavyovalishana mkituonyesha siri zenu enyi wana na humu mi simo.
Chokoraa nilipata pia nafasi ya kutembelea ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Mafia na hili ndilo jengo la "Muishiwa" huyu. Ha ha ha ha ha! Ati hapo inapopepea bendera ya kaya yetu hii, miaka kadhaa kabla ya 1961 ilipepea bendera ya "mkoloni". Simo humu miye.
Usiache kunitumia barua na hata kifurushi kutokea huko kwenu ughaibuni kwa anuani ifuatayo: Mheshimiwa Chokoraa wa Muhangaikaji wa Mlalahoi wa Pangupakavu wa Kabwela wa Mdanganyika, S.L.P .....Mafia, Pwani ya Wadanganyika. Pia biashara ya kuuza vocha inaendelea hapa na mimi nauliza haya makampuni ya simu yanalipia ushuru!!!!? Simo.
'Prezidenti' wa Wilaya, D.C ama ukipenda Mkulu wa Kaya wa Mafia ana ofisi zake hapa na hili lote ni jengo la ofisi za "muishiwa" huyu. Ati! Mtu mmoja jengo lote hili na mwalimu aliwahi kuuliza "...kwani mi tembo?". Na hii je!!!!!? Sihusiki naapa, simo.
Usitie shaka kuja na Njuluku, Pesa, Sinyingi, Hela, Chokoraa naita "Shekeli" zako huku kwetu maana hata sisi tunayo "Nyumba ya hela" na inayo "Ei tii Emu" inayofanya kazi saa 24 mfululizo. Sihusiki bado.
Uwanja wa ndege wa Mafia. Jengo hili halitumiki kwa sasa kwa sababu uwanja uko kwenye matengenezo makubwa ukitarajiwa kuwa na jengo la kisasa kabisa lakini hii ndiyo hali halisi miaka 50 baada ya uhuru. Sihusiki mimi humu..
'Muishiwa' Batuli, Diwani wa Kata ya Kirongwe, Kata ya Kaskazini Mafia akielezea jambo tulipokutana naye kwenye kijiji cha Jimbo huko Mafia. Wa kwanza kulia ni Dk. Kiwia, mtaalamu wa Uvuvi wenyewe twaita Fisheries. Nahusika kwani miye humu!!!? Simo.
Dk. Kiwia kutoka Fisheries, Ndg Makongoro mtaalamu wa mazingira, Chokoraa wa Muhangikaji wa Mlalahoi wa Pangupakavu wa Kabwela wa Mdanganyika, 'Muishiwa Diwani wa Kirongwe, Muishiwa Mwenyekigoda wa Kijiji cha Banja wakimsikiliza mwananchi akidadavua mada kwenye mkutano. Ha ha ha ha ha!!! Nijitoe na humu?. Simo.
No comments:
Post a Comment