Sunday, November 11, 2012

MSAFIRI KAFIRI

Ha ha ha ha ha ha ha! Naapa kwa hili hata kama mkigombana nami sitajari maana simo. Ati wadanganyika wanao msemo wao 'ma harufu' kwamba Msafiri Kafiri na mimi nauliza mwamaanisha nini enyi wana!?. Je! Kwamba msafiri kwa sababu ya shida za kushindwa kwenu kuwa ma mifumo bora ya usafiri, basi humlazimu kuweka kando imani ya dini yake na kuwa Kafiri!? Au kwamba ...........................
Wiki hii Chokoraa naye alikuwa "Kafiri"
Rubani wa 'boti' itokayo kisiwa cha Mafia kuelekea Nyamisati na mimi nauliza kama hawa waitwa Marubani, wa gari mwaita Madereva, mwendesha Baiskeli aitwaje!? Simo.

Hii ndiyo 'Festi Klass' na Chokoraa nauliza 'Thedi Klasi' ina hali gani!!!? Simo.
 Kwa ulingano huu wa idadi ya Abiria na Maboya, ajali ikitokea mtasema "Kazi ya Mungu haina makosa" kana kwamba na yeye ni mzembe kama ninyi. Simo humu naapa.
Mheshimiwa Diwani mtaasu wa kata ya Kilindoni naye alikuwamo kwenye msafara huu akielekea Dodoma kwenye mkutano mkuu wa  CCM

No comments:

Post a Comment