Wiki hii Chokoraa naye alikuwa "Kafiri"
Rubani wa 'boti' itokayo kisiwa cha Mafia kuelekea Nyamisati na mimi nauliza kama hawa waitwa Marubani, wa gari mwaita Madereva, mwendesha Baiskeli aitwaje!? Simo.
Hii ndiyo 'Festi Klass' na Chokoraa nauliza 'Thedi Klasi' ina hali gani!!!? Simo.
Kwa ulingano huu wa idadi ya Abiria na Maboya, ajali ikitokea mtasema "Kazi ya Mungu haina makosa" kana kwamba na yeye ni mzembe kama ninyi. Simo humu naapa.
Mheshimiwa Diwani mtaasu wa kata ya Kilindoni naye alikuwamo kwenye msafara huu akielekea Dodoma kwenye mkutano mkuu wa CCM
No comments:
Post a Comment