Kisiwani Mafia, linaonekana Gati la bandari ya kisiwa hiki likiendelea kujengwa. Hata hivyo Chokoraa nahoji juu ya uwepo wa 'utashi wa kisiasa' kulimaliza maana imekuwa muda mrefu tangu mradi huu kuanza. Simo humu namo.
Marafiki wawili katika viunga vya mji wa Mafia.
Meli ya Black Tiger ikiwa imepaki kwenye pwani ya Bandari Salama. Meli hii hutumiwa na kampuni ya Alphagroup kusafirisha mizigo yake kati ya Daressalaam na Mafia.
Ilikuwa ni siku ya Ijumaa, Chokoraa akitoka kisiwa cha Mafia kuelekea jiji la Daressalaam alipata nafasi ya kumshuhudia Mjasiriamali huyu akitoka kuchukua bidhaa kwa ajiri ya 'kibanda' chake akipishana na mabinti waliokuwa wakielekea kunako ibaada ya Ijumaa.
Mkoa wa Pwani pamoja na kuwa kandoni mwa Bahari una shida kubwa ya maji safi na salama kwa wakaazi wake wengi. Pembeni ya barabara kuu itokayo Mtwara kuelekea Dar, mkokoteni wa maji ukiwa umepaki kusubiri "oda" wa huduma zake. Dumu moja la maji huuzwa kati ya shilingi miambili na miatano kwa kutegemea uhitaji wa maji na eneo husika.
Kwenye eno la Mkuranga mkoani Pwani, biashara ya matunda kando ya barabara si jambo la kuuliza. Ha ha ha ha!! Chokoraa nilijichukulia matunda kwa ajiri ya kujenga afya.
Wilaya ya Mkuranga inavyo vituo vingi vya mafuta. Hapa ushushaji wa mafuta ulikuwa ukiendelea katika kukabiliana na tatizo la mafuta lililoikumba kaya yetu hii kwa wiki tatu mfululizo sasa. Hata hivyo ushushaji huo uliambatana na utoaji huduma jambo ambalo ni hatari kwa usalama wa watu na mali na sijui kama mamlaka husika zinajua na kuchukua hatua japo za miguu tena za makusudi. Simo.
Katika maeneo ambayo watu wamejenga holela na kuingia hadi ndani ya hifadhi ya barabara ni pamoja na mkoa wa Pwani. Maeneo na majengo mengi yamepigwa alama za X kuonyesha kwamba yamejengwa kinyume na sheria kwenye hifadhi ya barabara, lakini hii ndiyo Danganyika ya Wadanganyika walipa kodi, usishangae mwenye bango akaliandika upya na baadaye likapigwa tena X. Ni mchezo wa kuku na yai. Simo.
Nilipata pia nafasi ya kushuhudia Kondakta wa daladala akimuaga abiria wake huku gari likianza mwendo. Pamoja na hatari ya mchezo huu wa kuchungulia nje gari likitembea, makondakta wengi wanaonekana kutojali madhara yake na hapo ndipo Chokoraa ninapojitoa. Simo.
Atimaye tukasimama kwenye Bar ya dream Pub kwa ajiri ya kujipatia chochote kitu. Karibu tule kama jasho la mtu laliwa yakhe!!!!
Baada ya misosi, tulikipita pia kituo hiki ambacho kingali kikiendelea kujengwa.
Mkombozi wa Chokoraa katika safari zake za hapa na pale katika chakura chakura yangu majalalani. Ha ha ha ha ha!!! Jina la Kiswahili lakini hii siyo 'made in Kipawa bali made in China na hapo ndipo ninapojitoa, simo..
No comments:
Post a Comment