Wednesday, January 16, 2013

WADANGANYIKA: "GESI KWANZA, VYAMA BAADAYE". NAHUSIKAJE HUMU MIYE!!!?

Simo. Katika kile kinachoonekana kuwa hasira za Wadanganyika wa mkoa huu wa akina Njomba Nchumari, ntoto wa Chipoku kukataa suala la mtambo wa kurudufu Gesi kujengwa wilayani Kibaha Mkoani Pwani badala ya Mtwara, leo mkutano Mkubwa ulifanyika kwenye viwanja vya Bima na kuhudhuriwa na maelefu ya Wadanganyika walipa kodi na Chokoraa wa Muhangaikaji nilikuwapo kushuhudia hali ilivyokuwa japo simo, tena simo kabisaaaa. Ala!
"Kwa wale wote wanaotaka kumtumia salamu 'Mkulu wa kaya' kwamba wananchi wa Mtwara hawakatai gesi kutoka Mtwara bali wanakataa gesi kutoka ikiwa ghafi inueni mikono juu......". Matokeo yake ndiyo yaliyozaa picha hii. Nimo kwani humu?
 Hivi ndivyo wananchi walivyoonyesha hisia zao kwa 'Mkulu wa kaya' na Chokoraa nauliza; "Mkulu wa kaya unawasikia hawa?" ikiwa utaamua kuwapuuza mi sihusiki tena simo kabisaaaaaa.
Wadanganyika waliweka chini tofauti zao za dini, vyama na hata makabila na hapa kulikuwa na lugha moja tu, "Gesi kwanza, vyama baadaye". Simo naapa.
 Mwenyekiti wa Vijana wa Chama cha Wananchi (CUF) taifa Bw. Ahmad Katani alikuwa mmoja wa wazungumzaji kwenye mkutano huu na moja ya kauli zilizowakuna wasikilizaji wake ni hii "Hata akija mwenyekiti wa CUF taifa Prof. Ibrahim Lipumba na kusema Gesi iondoke, mtimueni.....". Nauliza humu Chokoraa nimo?.
 Hapa Bw. Katani akizungumza na Meza kuu.
"Mimi nimejitolea, naamini hata nikifa kwa kupigania maslahi na maendeleo ya watu nitaiona pepo pasipo shaka yoyote".
 Ilikuwa jioni muda wa watu kutoka makazini na hapa wanaonekana maafisa wa benki ya CRDB tawi la Mtwara wakijadiliana jambo pembezoni mwa uwanja wa mkutano. Simo humu namo.
 Pembezoni mwa barabara kuu eneo la Bima, wananchi wakisikiliza kilichokuwa kikiendelea kwenye mkutano wa CUF "Gesi kwanza vyama baadaye" Nahusikaje humu miye.
Mmoja wa wadau wa chokoraa blog naye alipitia hapa kusikia kisemwacho na wale wasemao na mimi sihusiki humu namo. Simo.
 Ha ha ha ha ha!!! Gheshi ra Porisi, ririkuwepo kuhakikisha usarama wa raia na mari sao". Simo humu.
 Mwenyekiti Ahmad akisisitiza jambo.
 Sehemu ya wananchi waliohudhuria.
Salamu za Pongezi zimetumwa kwa Jeshi la Polisi mkoani Mtwara kwa kutotumia mabavu kwenye mikutano hii ya wananchi na Chokoraa natuma pongezi zangu kwa Kamanda wa Polisi Mkoa Bi. Marry Nzuki. "Hongera Kamanda.

No comments:

Post a Comment